Ijumaa, 19 Julai 2013

ANGALIA THAMANI YAKO, YANINI KUMNG’ANG’ANIA ASIYEKUPENDA?



Ili mapenzi yaweze kuwa bora kwa kila aliye katika mahusiano, huwa ni vyema kila mmoja kuiona thamani ya mwenzake. Ukipenda kujiangalia mwenyewe  si ajabu mwenzako kupata hisia za kuwa humthamini wala humjali.
    Muunganiko wenu katika mapenzi maana yake tayari mmekuwa kitu kimoja. Katika mimi unaweka sisi.
Read more ...

KATIKA MAPENZI HAKUNA CHA KUPUUZIA, KUWA MAKINI



Mapenzi ni kitu cha tofauti kidogo. Umeshawahi kuona watu wakiwa ndani ya mapenzi moto moto? Umeshaona wanavyokuwa wakiwa pamoja? Hata kama wana miaka sitini ila wakati mwingine huwezi kutofautisha matendo yako na watoto.
   Hapo ndipo mapenzi yanapohitaji nafasi yake ili uweze kuyaelewa vizuri.
Read more ...

Jumanne, 16 Julai 2013

UNAYEMUACHA ANASTAHILI?



Uamuzi unaochukua leo ndiyo wenye kuweza kukusababishia furaha au majuto baadaye. Mambo mengi yaliotokea leo ni matokeo ya kile ulichokiamua jana. Iko hivyo na  Hata katika mapenzi hali ni hiyo hiyo.
    Uzuri wa mahusiano yako ya leo umeamuliwa na uamuzi mzuri wa kusikiliza hisia zako na kuamua kuwa na huyo uliye naye leo.
Read more ...

BILA UVUMILIVU UTAACHA KILA SIKU, KUWA MAKINI KATIKA HILI



Ukiwa mtu wa kuangalia mambo kwa juu juu basi kila kitu kwako kitakuwa kigumu. Kusoma unaweza kuona ni kugumu, kufanya kazi kugumu, hata kusubiri mshahara unaweza kuona ni kugumu.
  Urahisi kwako unaweza kuwa katika kutumia pesa, pengine  na kula tu. Ila watu waelevu na wenye uvumilivu kwako kila kitu kinaweza kuwa tofauti na wewe.
Read more ...

Jumapili, 14 Julai 2013

HATAKI KUBADILIKA KWA SABABU HII



Uhusiano wa mapenzi ni muunganiko wa hiyari wa watu wawili wenye kupendana,kukubaliana na walio tayari kuvumiliana na kurekebishana pale inapobidi. Hiyo ni moja kati ya tafsiri rahisi ya uhusiano wa mapenzi.
    Mtu yoyote aliyekuwapo katika mahusiano anatakiwa kuwa tayari kumsikiliza mwenzake, kumvumilia na kubadilika kitabia pale inapopaswa kuwa hivyo.
Read more ...

Ijumaa, 12 Julai 2013

JIULIZE HAYA KWA FAIDA YA MAPENZI YAKO



 Kupendana kwa dhati ni nguzo imara  inayofanya mapenzi baina ya wapendanao yaweze kuwa imara na madhubuti. Wanaopendana kwa dhati wanasikilizana, kuhesimiana na kila mmoja kuwa na hamu na shauku na mwenzake.
   Katika mapenzi hivyo ni vitu muhimu sana. Ili mapenzi yaweze kustawi heshima inabidi iwepo baina ya wahusika. Ili kila mmoja aweze kuwa na furaha na faraja katika mahusiano inabidi miongoni mwao kuwepo na hamu na shauku. Mmoja akikosa hali hii mapenzi hukosa ladha. Si ajabu kuona mwingine akianza kuhisi anajipendekeza kwa mwnenzake au kuona akikosa raha kabisa ndani ya mahusiano hayo.
   Wewe uko vipi kwa mpenzi wako?
Read more ...

UNAMJUA ULIYENAYE? USIKIMBILIE KUJIBU



Moja kati ya vitu vinavyowafanya vijana wengi washindwe kufurahia maisha yao ya kimahusiano ni hali ya kwenda jino kwa jino na wapenzi wao. Vijana wengi wanajikuta kila siku wakiingia katika matatizo na  wenzi wao kwa sababau hii.
  Anataka ajue kila mpenzi wake anayewasiliana naye,anataka kila safari ya mpenzi wake aifuatilie mpaka mwisho. Katika hali hii ni lazima tu utajikuta ukiingia katika migogoro isiyo na lazima na mpenzi wako.
   Wakati wewe ukiona uko sahihi kwa msemo wa abiria chunga mzigo wako, mwenzako ataona unafanya dunia isiwe mahala huru kwake. Ndiyo, utakuwa unamnyima uhuru wake. Kuwa naye katika mahusiano haina maana kuwa katengana na dunia nzima.
  Nakubali kuwa inafaa awe na udhibiti wa kuwa na wewe. Ajue tofauti ya sasa na zamani, ila pia jua ana marafiki na watu wake wengine wakaribu hivyo ni lazima tu awe na mawasilaino nao. Huko katika shule na kazini ni lazima tu alikuwa na watu muhimu wa kumsaidia katika masuala mbali mbali ya kimaisha, sasa kuwa na wewe isiwe ndiyo mwisho wa urafiki wao. Suala linalotakiwa hapo ni kuachana na wale tu wanaoonekana kama akiwa nao basi mahusiano yenu kuwa imara ni ndoto za mchana. Unamjua mpenzi wako vizuri?
         Usimbilie kujibu,fikiri kwanza.
Read more ...