Moja kati ya
vitu vinavyowafanya vijana wengi washindwe kufurahia maisha yao ya kimahusiano
ni hali ya kwenda jino kwa jino na wapenzi wao. Vijana wengi wanajikuta kila
siku wakiingia katika matatizo na wenzi
wao kwa sababau hii.
Anataka ajue kila mpenzi wake anayewasiliana
naye,anataka kila safari ya mpenzi wake aifuatilie mpaka mwisho. Katika hali
hii ni lazima tu utajikuta ukiingia katika migogoro isiyo na lazima na mpenzi
wako.
Wakati wewe ukiona uko sahihi kwa msemo wa
abiria chunga mzigo wako, mwenzako ataona unafanya dunia isiwe mahala huru
kwake. Ndiyo, utakuwa unamnyima uhuru wake. Kuwa naye katika mahusiano haina
maana kuwa katengana na dunia nzima.
Nakubali kuwa inafaa awe na udhibiti wa kuwa
na wewe. Ajue tofauti ya sasa na zamani, ila pia jua ana marafiki na watu wake
wengine wakaribu hivyo ni lazima tu awe na mawasilaino nao. Huko katika shule
na kazini ni lazima tu alikuwa na watu muhimu wa kumsaidia katika masuala mbali
mbali ya kimaisha, sasa kuwa na wewe isiwe ndiyo mwisho wa urafiki wao. Suala
linalotakiwa hapo ni kuachana na wale tu wanaoonekana kama akiwa nao basi
mahusiano yenu kuwa imara ni ndoto za mchana. Unamjua mpenzi wako vizuri?
Usimbilie kujibu,fikiri kwanza.
Read more ...