Alhamisi, 11 Julai 2013

MAHUSIANO YAKO NI YA AINA GANI?



      Upo katika muundo upi wa mapenzi? Wewe na mpenzi wako mahusiano yenu yakoje? Niyafuraha na upendo au ni yale yanaokutegemea zaidi ili yawepo?
     Ni ndoto ya kila mmoja kuwa katika mahusiano yaliyotawaliwa na furaha na amani. Mahusiano yenye kila aina ya amani na uchangamfu.
     Ila kwa bahati mbaya ni wachache sana walifanikiwa katika hilo. Wengi mahusiano yao ni kizungumkuti. Visa na maudhi kwa kwenda mbele. Amani na upendo wamebaki kuvisikia kutoka kwa wengine, kwao ni kitendawili. Wewe upo katika mahusiano ya namna gani?
    Unaridhika na jinsi mapenzi wako alivyo kwako. Japo huenda akawa hakupi fedha kutokana na sababu kadhaa lakini ni kweli anaonesha kukujali? Anakupigia simu mara ngapi? Hata kama salio hana je, hata kuku’beep’ tu inashindikana!
    Je, wewe ndiyo kila siku umekuwa mwenye kutaka kuonana naye huku yeye akiwa hana habari? Upo katika mapenzi ya namna hiyo?
     Mpenzi wako anakupa sababu yakufurahi au ndiyo vile kila siku huwa unajutia uamuzi wa kuwa naye. Kila siku yeye kwako anahitaji fedha ukiacha kumpa basi humpendi. Je, mpenzi wako ni wa aina hiyo?
    Jamani, tunapaswa kuelewa kuwa mapenzi ni raha na faraja sana. Unapokuwa hauko katika mapenzi ya namna hiyo unapaswa kujiuliza
    Hapo huenda ukawa umedondokea katika mikono ya wasanii wa mapenzi. Ambao wao kwao mapenzi huwa na misimu kama ligi za mpira. Leo anaweza kujifanya anakupenda sana ila kesho hata ‘sms’ yako hajibu. Na akijibu basi ni kwa maneno ya mkato mno. Kama siyo ‘thanks, basi itakuwa ‘poa tu’. Ni vyema ukajiuliza muundo wa mapenzi uliyopo ili kuweza kuchukua hatua zinazofaa kabla mambo hayajazidi kuharibika zaidi.
    Kuwa na mpenzi ambaye hakupi raha na furaha ni kupoteza muda tu na kujipa ‘stress’ za bure. Ni wewe ambaye kila siku umekuwa ukilia tu. Ni wewe ambaye kila siku unaomba msamaha kwa makosa ambaye anakufanyia wewe.Hayo mapenzi kweli?
    Kulilia penzi la mtu asiyeonesha kukujali wala kutambua thamani yako ni kujiingiza katika utumwa. Utumwa ambao mwisho wake nikukuachia majuto makuu ya kukaa kwa muda mrefu katika mahusiano na mtu ambaye mwisho wenu utakuwa ni ule ambao hukuutegeamea. Mwisho wa kutengana haliyakuwa huku ukiwa amekupotezea muda pengine na thamani yako machone pa wengi.
    Yangalie vizuri matendo yake juu yako. Angalia maneno yake. Je, yanakufanya ufurahi? Ni matendo ya wapendanao?
     Maisha yako yanahitaji furaha ili uweze kuishi kwa amani. Na asilimia kubwa ya furaha inatakiwa kusababishwa na mpenzi wako. Sasa vipi unapokuwa katika mahusiano na mtu anayekukera na kukufanya ujute? Kweli utakuwa na furaha? Ni kitendawili. Kama si kuambulia msongo wa mawazo pamoja na sura kukunjika kwa hasira za kila siku!
    Kuwa katika mahusiano na mtu ambaye hapendi kukuona na furaha ni kujimaliza. Kwa sababu atafanya utendaji wako wa kazi kushuka,uchangamfu ukupotee kutokana na karaha zake. Ni ngumu mno kupata hata maendeleo kama huwi mtu wa furaha na uchangamfu. Na pia ni ngumu sana kuwa mtu wa furaha kama uko katika mahusiano na mtu wa vituko na visa visivyo kwisha.
    Kila siku unamwambia neno moja. Kila siku wewe ndiye unamtafuta. Chunguza vizuri mahusiano yako. Kisha jibu swali hili, Upo katika mahusiano ya namna gani?
         ramadhanimasenga@yahoo.com



            




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni